Page Nav

HIDE

Breaking News:

latest

HESABU ZA YANGA MATATA SANA

MWENYEKITI wa kamati ya uhamasishaji kwa ajili ya kuichangia Yanga, Antony Mavunde amewataka wananchi kuendelea kuichangia timu ili kufiki...


MWENYEKITI wa kamati ya uhamasishaji kwa ajili ya kuichangia Yanga, Antony Mavunde amewataka wananchi kuendelea kuichangia timu ili kufikia malengo ambayo wamejiwekea.

Mavunde amebainisha mipango iliyopo kwa sasa ambayo ni kufanikiwa kuchangia zaidi ya shilingi 1.5 bilioni kutoka wa wanachama na mashabiki wa Yanga mikoa yote nchini.

Yanga kwa sasa inajiendesha kutokana na nguvu ya michango ya wanachma kutokana na kupita kipindi cha mpito.

Ili kuichangia Yanga kupitia mitandao ni kupitia namba hii *150*01# kisha chagua namba 4 lipa bili, hatua inayofuata chagua namba 3 weka namba ya kampuni ambayo ni 101120, kumbukumbu namba weka namba 1 kisha weka kiasi kisipungie mia tano, weka namba ya siri kuhakiki kisha utapokea Ujumbe wa kuthibitisha.

No comments