Page Nav

HIDE

Breaking News:

latest

SIMBA YATAKA WATU ELFU SITINI TAIFA KUWAUA VITA

Uongozi wa klabu ya Simba umetangaza viingilio vya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Barani Afrika kati yao na AS Vita utakaopigwa Jumamosi ya wi...


Uongozi wa klabu ya Simba umetangaza viingilio vya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Barani Afrika kati yao na AS Vita utakaopigwa Jumamosi ya wiki hii jijini Dar es Salaam

Kuelekea mechi hiyo, Manara ametaja viingilio kuwa vitakuwa ni shilingi 3000 kwa mzunguko na Orange, VIP B 10,000 na VIP A 20,000 huku Platnums itakuwa ni 100,000.

PAKUA APPLICATION YETU   CLICK TO DOWNLOAD

Tiketi ya Platnums itampa usafiri shabiki kwenda Uwanjani akitokea Serena Hotel mpaka Uwanjani na atakaa sehemu ambayo itaambatana na vinywaji huku akipewa na jezi.

Simba inaedna kucheza na Vita ikiwa na kumbukumbu mbaya ya kufungwa maba0 2-0 na JS Saoura katika mchezo wa mwisho uliopigwa huko Bechar, Algeria.

PAKUA APPLICATION YETU   CLICK TO DOWNLOAD


Mbali na viingilo, Manara amewataka mashabiki Simba kujitokeza kwa wingi kwenye mchezo huo kwani lengo lao kubwa ni kuhakikisha wanashinda na si kingine.

Manara ameeleza uwepo wa mashabiki na haswa wakifika 60,000 itakuwa jambo jema katika kuleta hamasa kwa wachezaji siku hiyo.

PAKUA APPLICATION YETU   CLICK TO DOWNLOAD


Mechi hiyo inayosubiriwa kwa hamu na wadau wa mpira hapa nchini, itapigwa majira ya saa 1 za usiku katika Uwanja wa Taifa.

No comments