Mwanamitindo Hamisa Mobetto amesema kuwa alikuwa tayari kuwa mke wa pili wa Diamond Platnumz iwapo angemuoa Zari The Bosslady. Hamisa a...
Mwanamitindo Hamisa Mobetto amesema kuwa alikuwa tayari kuwa mke wa pili wa Diamond Platnumz iwapo angemuoa Zari The Bosslady.
Hamisa akizungumza kwenye kipindi cha Mambo Mseto cha Citizen Radio nchini Kenya, amesema hata angeolewa na akawa mke wa kwanza hawezi kumkataza mume wake kuoa mwanamke mwingine.
"Nilimuuliza akasema Muislam anaweza kuoa wanawake wengi, Yeah hata kama ikitokea nimeolewa mke wa kwanza, ikatokea anataka kuongeza mwanamke mwingine am ok with that, nilikuwa tu sawa kwa sababu ni kitu ambacho nimeshakipitia," amesema Hamisa.
No comments