Ikiwa ni baada ya kuondolewa kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika, Kocha Mkuu wa Simba Mbelgiji, Patrick Aussems amesema kuwa hasira zote ...
Ikiwa
ni baada ya kuondolewa kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika, Kocha Mkuu wa
Simba Mbelgiji, Patrick Aussems amesema kuwa hasira zote wanazihamishia
kwenye Ligi Kuu Bara na Kombe la FA.
Simba
iliondolewa kwenye na UD Songo ya nchini Botswana kwenye Raundi ya
Awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kufungana na 1-1 kwenye mchezo
wa pili wa marudiano uliopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es
Salaam.
Timu
hiyo kwenye mchezo wa kwanza uliopigwa Beira, Msumbiji ilitoka suluhu
na Songo kabla ya kurejeana na kutoka sare hiyo ya bao 1-1 ambayo
keshokutwa Alhamisi itakuwepo uwanjani ikicheza mchezo wake wa ligi
dhidi ya JKT Tanzania.
Akizungumza, Aussems alisema kuwa hasira zote anazihamishia kwenye
ligi na Kombe la FA na kikubwa kuhakikisha wanachukua makombe.
“Nawaomba mashabiki kuendelea kutuunga mkono katika ligi na Kombe la FA baada ya kutolewa kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.
“Hayakuwa
malengo yetu kuondolewa katika hatua hii, bahati haikuwa yetu kwani
timu ilitengeneza nafasi nyingi za kufunga lakini tulishindwa kuzitumia.
“Hivyo,
tunarudi kwenye ligi na kikubwa mashabiki waendelee kujitokeza uwanjani
kama mwanzoni kwa ajili ya kutupa sapoti ili tufanikishe malengo
yetu,”alisema Aussems.
No comments