Page Nav

HIDE

Breaking News:

latest

NADO ATUPIA KAMBANI AZAM IKIITWANGA KMC 1-0 UWANJA WA UHURU

Azam FC imefanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya KMC FC, mechi ikichezwa kunako Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. Mech...


Azam FC imefanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya KMC FC, mechi ikichezwa kunako Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Mechi hiyo iliyokuwa ya aina yake kwa timu zote mbili kucheza soka la kuvutia, ulimshuhudia mshambuliaji Idd Suleiman Nado akitupia kambani bao hilo katika dakika ya 15 ya mchezo.

Bao hilo limefanikiwa kudumu kwa dakika zote 90 mpaka mpira unamalizika matokeo yakiwa ni 1-0.

Timu hizo mbili zimekutana kwa mara ya kwanza katika ligi tangu kumalizika kwa msimu uliopita.

No comments