Page Nav

HIDE

Breaking News:

latest

TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA LEO JUMANNE YA AGOSTI 27 2019

Huenda Manchester United ikasubiri ukaguzi wa mchezaji wa kiungo cha mbele raia wa Ufaransa Anthony Martial, mwenye umri wa miaka 23, kabl...


Huenda Manchester United ikasubiri ukaguzi wa mchezaji wa kiungo cha mbele raia wa Ufaransa Anthony Martial, mwenye umri wa miaka 23, kabla ya kuruhusu uhamisho wa mkopo wa mchezaji wa kimataifa wa Chile Alexis Sanchez, mwenye umri wa miaka 30, kwenda Inter Milan. (Guardian)

Paris St-Germain imeambia Real Madrid itatafakari kumuuza mchezaji wa Brazil wa kiungo cha mbele Neymar, mwenye umri wa miaka 27, iwapo mchezaji wa klabu hiyo ya Uhispania mwenye miaka 19 na mshambuliaji wa Brazil Vinicius Jr iatakuwa sehemu ya makubaliano ya kudumu. (AS)

Wakurugenzi wa Barcelona wamekutana Jumatatu kujadili ombi la mchezaji wao wa zamani Neymar. (Marca)

Huenda Inter Milan ikamgeukia mchezaji wa kiungo cha mbele wa Manchester City Wilfried Bony, mchezaji huyo wa Ivory Coast mwenye miaka 30 kwa sasa haichezei klabu yoyote baada ya kuachiwa na Swansea msimu wa joto. (Goal.com)

Mchezaji wa kimataifa wa Serbia Nemanja Matic, mwenye umri wa miaka 31, ameitisha mazungumzo na meneja wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer baada ya kuipoteza nafasi yake ya kwanza huko Old Trafford. (Mirror)

Arsenal ipo tayari kumruhusu mchezaji wa kimataifa wa Uhispani Nacho Monreal kujiunga na Real Sociedad wiki hii iwapo mchezaji huyo wa miaka 33 na mchezaji wa kiungo cha ulinzi ataomba kuondoka. (Sun)

Javi Gracia anapigania kuokoa nafasi yake kama meneja wa Watford baada ya kuanza msimu wa ligi kuu England kwa kushindwa mara tatu. (Telegraph)

Mshambuliaji wa Chelsea Tammy Abraham anaelekea kupata mkataba mpya ambao huenda ukaongeza zaidi ya mara mbili malipo ya mchezaji huyo wa miaka 21 raia wa England ya £50,000 kwa wiki(Telegraph)

Wawakilishi wa Christian Eriksen hawatofikiria pendekezo la mkataba wa Tottenham la malipo ya £200,000 kwa wiki na mchezaji huyo wa miaka 27 ambaye mkataba wake hivi sasa unamalizika msimu ujao wa joto anatumai kupata uhamisho kwenda Uhispania. (Mirror)

Eriksen ni kama amejiuzulu kusalia Tottenham katika kipindi kifupii, huku ndoto yake ya kujiunga na Real Madrid au Barcelona msimu huu wa joto ikishindwa kufanikiwa. (Mail)

Winga wa Celta Vigo Pione Sisto, mwenye umri wa miaka 24, anakaribia kujiunga na Torino baada ya uhamisho kwenda Aston Villa kutofanikiwa. (Marca)

Mabingwa wa Italia Sampdoria wanataka kumsajili winga wa Swansea anayeichezea timu ya taifa ya Ghana Andre Ayew, mwenye umri wa miaka 29, kwa mkopo kabla ya kufungwa kwa dirisha la uhamisho Ulaya (Star)

No comments