Yule kiungo mkabaji wa Simba, Jonas Mkude leo alikosekana kwenye mazoezi ya timu hiyo yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Gymkhana, Posta...
Yule
kiungo mkabaji wa Simba, Jonas Mkude leo alikosekana kwenye mazoezi ya
timu hiyo yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Gymkhana, Posta jijini Dar es
Salaam.
Timu hiyo inatarajiwa kucheza mchezo huo kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam kuvaana na JKT Tanzania.
Akizungumza , Kocha Mkuu wa timu hiyo Mbelgiji, Patrick Aussems
alisema kuwa alishindwa kufanya mazoezi hayo baada ya kupata homa.
Aussems
alisema kuwa kiungo huyo atarejea uwanjani mara baada ya kupona homa
hiyo aliyoipata ikiwa ni siku moja tangu waondolewe katika michuano hiyo
mikubwa Afrika.
Aliongeza
kuwa, tayari ameanza maandalizi ya timu hiyo kwa ajili ya mchezo wao
dhidi ya JKT kwa kumuandaa mbadala wake kutokana na yeye kutokuwepo
kabisa katika mchezo huo.
“Mkude
atakosekana katika mchezo wetu wa Alhamisi tutakapokuwepo uwanjani
tukicheza mchezo wetu wa kwanza wa ligi baada ya kupata homa.
“Leo
hakuwepo mazoezini kutokana na kuendelea na matibabu yatakayomrejesha
haraka uwanjani kwa ajili michezo ijayo ya ligi,” alisema Aussems.
No comments