Msanii wa Bongo Fleva, TID amemkosoa vikali Harmonize kwa kile alichodai kuwa amekuwa akiiga muziki wa Nigeria. TID amesema ...
Msanii wa Bongo Fleva, TID amemkosoa vikali Harmonize kwa kile alichodai kuwa amekuwa akiiga muziki wa Nigeria.
TID amesema kitu hakikuwepo kipindi cha nyuma na Bongo Fleva ilikuwa inafanya vizuri lakini kilichopo sasa ni kuiga muziki wa Nigeria.
"Hizi sound na Kinigeria mimi nilikuwa sizijui, 2010 hizi zilikuwa hazipo hizi, we have the best sound Africa, sisi na Wakenya," amesema.
"Ulikuwa unasikia Bongo Fleva na Wakenya huko South Africa, Korra, tunatamba sisi. Image sasa hivi tunamsikia Harmonize anakopi , kitu gani unafanya, unataka kujiunga na Wanigeria au?," TID ameiambia Metro
Licha ya kufanya kolabo na wasanii kadhaa wa Bongo Fleva, Harmonize amefanya kazi na wasanii wa Nigeria kama Yemi Alade, Reekado Banks, Korede Bello na wengineo
RNGM blog


No comments