Page Nav

HIDE

Breaking News:

latest

WCB hawana mgogoro wowote na Rich Mavoko - BASATA

Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) limeweka wazi kuwa litakuwa na kikao cha pamoja kati ya WCB na Rich Mavoko. Akizungumza ofisini kwake...









Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) limeweka wazi kuwa litakuwa na kikao cha pamoja kati ya WCB na Rich Mavoko.

Akizungumza ofisini kwake leo Katibu Mtendaji wa Basata, Godfrey Mngereza amesema kuwa pande hizo mbili hazina mgogoro wowote na lengo la Baraza ni kumaliza tofauti zilizopo.


"Kimsingi tutakuwa na kikao kingine cha pamoja kati ya upande wa Rich Mavoko na upande wa Wasafi,' amesema.

"Wasafi hawana mgogoro wowote na Rich Mavoko, kwa hiyo lengo la baraza nikukutanisha pande hizo," amesema 


Kauli ya BASATA inakuja mara baada ya Diamond na viongozi wa WCB kufika ofisi za baraza hilo kujadili suala la Rich Mavoko ambaye hapo awali alifika hapo kueleza kile alichodai mkataba kati wake na WCB ulikuwa wa kinyonyaji.


RNGM blog

No comments